Ruthu 2:14-18 - 16-07-2026
Alhamisi asubuhi tarehe 16.07.2026
Ruthu 2:14-18
[14]Tena wakati wa chakula huyo Boazi akamwambia, Karibu kwetu, ule katika mkate wetu, na ulichovye tonge lako katika siki yetu. Basi akaketi pamoja na wavunaji, nao wakampitishia bisi, naye akala akashiba, hata akasaza.
[15]Naye alipoinuka tena ili aende kuokota masazo, huyo Boazi aliwaagiza vijana wake akisema, Mwacheni aokote hata kati ya miganda, wala msimkemee.
[16]Tena mtoleeni kidogo katika matita na kukiacha, na akiokote, wala msimkataze.
