July 2026

Ruthu 2:14-18 - 16-07-2026

Alhamisi asubuhi tarehe 16.07.2026

Ruthu 2:14-18

[14]Tena wakati wa chakula huyo Boazi akamwambia, Karibu kwetu, ule katika mkate wetu, na ulichovye tonge lako katika siki yetu. Basi akaketi pamoja na wavunaji, nao wakampitishia bisi, naye akala akashiba, hata akasaza.

[15]Naye alipoinuka tena ili aende kuokota masazo, huyo Boazi aliwaagiza vijana wake akisema, Mwacheni aokote hata kati ya miganda, wala msimkemee.

[16]Tena mtoleeni kidogo katika matita na kukiacha, na akiokote, wala msimkataze.

1 Yohana 3:17-20 - 15-07-2026

Jumatano asubuhi 15.07.2026;

1 Yohana 3:17-20

17 Lakini mtu akiwa na riziki ya dunia, kisha akamwona ndugu yake ni mhitaji, akamzuilia huruma zake, je! Upendo wa Mungu wakaaje ndani yake huyo?

18 Watoto wadogo, tusipende kwa neno, wala kwa ulimi, bali kwa tendo na kweli.

19 Katika hili tutafahamu ya kwamba tu wa kweli, nasi tutaituliza mioyo yetu mbele zake,

20 ikiwa mioyo yetu inatuhukumu; kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mioyo yetu naye anajua yote.

Upendo wa Mungu na utawale;

Utangulizi;

1 Samweli 20:35-42 - 13-07-2026

Jumatatu asubuhi tarehe 13.07.2026

1 Samweli 20:35-42

35 Hata asubuhi Yonathani akatoka kwenda shambani wakati ule alioagana na Daudi, na mtoto mdogo alikuwa pamoja naye.

36 Akamwambia mtoto wake, Piga mbio, ukaitafute mishale niipigayo. Na yule mtoto alipokuwa akipiga mbio, akapiga mshale, ukapita juu yake.

37 Na mtoto alipofika penye ule mshale alioupiga Yonathani, Yonathani akampigia mtoto kelele, akasema, Je! Mshale si huko mbele yako?

Matangazo ya usharika tarehe 12 Julai 2026

DAYOSISI YA MASHARIKI NA PWANI  

MATANGAZO YA USHARIKA  TAREHE 12 JULAI, 2026

SIKU YA BWANA YA 6 BAADA YA UTATU

NENO LINALOTUONGOZA NI:

UPENDO WA MUNGU NA UTAWALA”

1. Tunawakaribisha wote tumwabudu Mungu wetu katika Roho na kweli.

2. Wageni:Joseph Jackson kutoka Arusha.

3. Matoleo ya Tarehe 05/07/2026

Tunamshukuru Mungu aliyetupa afya ya kumwabudu na utayari wa kumtolea kwa hiari mali alizotupa kwa kazi yake.

NAMBA YA SADAKA KWA NJIA YA MTANDAO:

- 0757 391174 - KKKT AZANIA FRONT