Wanawake wa Usharika wa Azania Front Wahudhuria Semina
Wanawake wa Usharika wa Kanisa Kuu Azania Front Cathedral hivi karibuni walihudhuria semina ya kiroho na kiuchumi. Semina hiyo ya siku moja ilifanyika tarehe 30/4/2022 katika kituo cha Consolata Mission Centre, Bunju Dar Es Salaam na kuhudhuriwa na mamia ya washarika wanawake wa Usharika wa Kanisa Kuu Azania Front Cathedral.
Semina hiyo iliyokuwa na lengo la kuwaweka wanawake pamoja kwa ajili ya kupata mafundisho ya kiroho na kiuchumi, iliandaliwa na viongozi wa Umoja wa wanawake usharikani wakishirikiana na uongozi wa Usharika.
