October 2021

Wenza wa Wachungaji DMP watoa shukrani

Wenza wa wachungaji wa KKKT Sharika za Dayosisi ya Mashariki na Pwani (DMP) wametoa shukrani katika Usharika wa Kanisa Kuu Azaniafront Cathedral kama sehemu ya kuadhimisha miaka nane tangu kuanzishwa kwa vicoba ambayo mpaka sasa ina akiba ya takriban Tsh 400,000,000/-. Pia vicoba hiyo hivi karibuni imechaguliwa kuwa vicoba bora katika nyanja ya uwekezaji nchini Tanzania.